Friday, March 5, 2021

ONA JINSI KUNGURU WANAVYOOMBOLEZA MISIBA YAO

KUNGURU NA MAISHA YAO



Unaweza sema ni wasumbufu,Vidokozi,kukuangushia kinyesi kisha wakawa kama wanafurahia tukio kwao ni jambo
la kawaida saaana,na hawa ndege aisee ni wachukuzi wa chochote kitakachokuwa mbele yao.
Lakin hawa jamaa bana huenda ndo ndege wenye Akili nyingi kuliko wengine,Na hawafanyi kitu bila kujihakikishia 
kama ni hatari au laaah,Ndio huenda ni kweli niyasemayooo,Embu jaribu Siku mfukuze kwa kutishia kama unamrushia jiwe
Akishagundua tu kwamba hata jiwe lenyewe huna,Basi hawez kukimbia kaamwe atakaa hapo hapoo,ila Ukishika kweli jiwe basi Atakimbia



Wednesday, February 17, 2021

ZIJUE FAIDA ZA LIMAO

 HILO NDO LIMAO

Muhimu ni kuliandaa vizuri na kufata maelekezo

Leo ningependa kuwapa kitu tofauti kidogo
Kila mtu analijua limao na faida zake zipo nyingi  tu, ikiwemo kutumika kutengenezea dawa za tiba mbalimbali
mfano tiba ya ngozi,tiba ya kifua na nyingine nying nyingnezo.lakini leo nakuonesha  faida 
tatu tu kutoka kwenye limao
Lakufahamu kwanza limao ni tunda lenye umaji maji wa acid, yaani ni tunda lenye citric acid
na uwingi wa vitamin c

Kukata harufu ya kikwapa
Huu ni mbadara mkubwa wa matumizi ya deodorant ambazo ni chemical na pia
hufubaza nguo katika maeneo ya kwapa kwa kiwango kikubwa
unachotakiwa kufanya ni kukata kipande kidogo tu cha limao na kupaka kwapani
subiria bila kusafisha kwa dakika tano mpaka kumi kisha nawa au nenda kaoge
hutokaa na kusikia haruf ya kikwapa zaidi ya siku tano. ,unaweza paka tena baada hata ya siku tatu
usitumie njia hii baada ya kushave

Unaweza fanya hivyo hvyo katika maeneo mengine ya mwili ambayo unaona 
yanatoa harufu mbaya,unaweza fanya hayo bila shida yoyote na ikakupa matokeo
 mazuri tu.
Kusafishia aina zote za chuma
Kusafisha vitu vya chuma ambavyo uchafu umegandiaa, mfano ule uchafu wa jikoni
uchafu unaonata ,uliochanganyika na mafuta mfano mafuta mafuta ya samaki

Katika hili kuna cha ziada inabd uwe nacho ,baking powder

Andaa baking powder hiz za kawaida za Simba, andaa na limao lako.
Sambaza unga wa baking powder katika eneo unalotaka kusafishaa,kamua limao 
katika chombo kisha umiminie,au kamulia limao moja kwa moja katika sehem uliyosambaza
unga wa baking powder  ,subiria kwa dakika tano,kisha anza kusafisha kwa brush tu la kawaida la vyombo

ukimaliza hapo unaweza ukafuta tuu na kitambaa safi na sabuni

Kulainishiaa maeneo ya mwili
Tatu ni katika kulainisha maeneo katika mwili ambayo kidoogo yamekakamaa
mfano kama  nyayo za miguu yako zimekakamaaa ,unaweza kutumia limao kufanya unyayo ukawa
soft/laini  tena
unachotakiwa kufanya ni rahisi tu chagua siku au muda ambao hauna shughuli ya kufanya
angalau kwa sekunde 30,kata vipande vipande vidogo dogo  vya malimao na maganda yake
kisha weka chini ya unyayo  valia na soksii tulia kwa dakika 30 ,unaweza tumia muda huo kuangalia movie 
ama maigizo mbali mbali  baada ya hapo toa kanawe miguu yako ,utanishukuru baadaae 

Kama vitamin C katika kupambana na kinga ya mwili
Limao lina kiwango kikubwa cha vitamin C inayoweza kusaidiia kuinua kinga ya mwili na kupambana na maradhi aina nying 
yanayosababishwa na upungufu wa vitamin C ikiwemo mafua

MJUE MWANAMKE ALIYEKUWA NA NYWELE ZENYE VICHWA VYA NYOKA

MEDUSA


 

Mwanamke wa kutishaa,Mwanamke mwenye kichwa chenye Vichwa vya nyoka katika kila unywele ulio kichwani mwake

Lakin unaweza kuamini  mwanamke huyu alikuwa ni mzurii kiasi cha kumvutia kila mwanamme amtazamae ?

Huyo ni medusa ,ungana nami kwenye stori hii..

Habari yake inaanzia miaka elfu na elfu iliyopita katika hadithi za kale za kigiriki

 Medusa akifahamika kwa jina lingine kama gorgons,mwanamke mrembo mwenye nywere za dhahabu 

Wakiwa wadada wa tatu Sthenno, Euryale pamoja na yeye medusa.Urembo wake ndio ulimpa umaaarufu kuliko dada zake 

wengine wote

Medusa aliponzwa na uzuri wake ,mmoja ya waliochanganyikiwa na uzuri wake alikuwa Poseidon,

Poseido kwa hadithi za kale za kigiriki walikuwa wakimjua kama Mungu wao wa Baharii na alama yake kubwa ni kutembea 

na mkuki wenye alama ya reki kwa mbele,



Poseidon alimbakaa Medusa katika Hekalu lenye heshima kubwa ,hekalu lilokuwa linamilikiwa na Athena.

Baada ya Athena kugundua kuna uchafu umefanyika katika hekalu lake,na uchafu uliofanyika kwa mwanamke Mrembo Medusa

kwa ghadhabu aliamua kuzibadilisha kichwa chenye nywele nzuri za medusa kuwa vichwa vya nyoka hatarii

huku akiwa na mkia mkubwa wa nyoka



Ikawa mwanaume yeyote atakayemuangangalia Medusa basi hugeuka na kuwa jiwe la udongo,akawa si medusa mrembo tena,

Ila ni medusa mwenye Hasira na Wanaume,Mwanamke mwenye hasira ya Kila anaemuangaliaa Usoni

Kiumbe yoyote atakayemuangalia Medusa hugeuka jiwe la udongo

Hapo ndo mwanzo wa Medusa kuishi kuzimu chini ya miamba yenye joto kalii,kujiepusha na muunganiko wa watu.



Medusa aliua watu wengi waliomkalibiaaa,wakitaka kukata kichwa chake,na lengo lao kubwa kukitumia hiko kichwa 

katika kuangamiza viumbe wengine wasumbufu ,kama wanyama wakubwa,kuulia wababe wengine wa vita na kadhalikaa

Hatimae Medusa Aliuawa na kukatwa kichwa na Mtu aliyejulikana kama  Perseus

 Perseus alikuwa mtoto wa binti wa mfalme Argos aliyeingiliwa kimwili na Zeus,ambae katika hadithi za kale za wagiriki

walikuwa wakimjua kama Mungu wa Anga na Radi

Perseus ndiye pekee aliyefanikiwa kumuua medusa ,perseus alipambana na Medusa bila kumuangalia uson,. alitumia kioo


kilingokuwepo kwenye ngao yake mpaka akafanikiwa kukata kichwa cha medusa,

Kichwa cha medusa kilitumika kama ngao au kinga ya vitu au viumbe wa Baya,na mpaka sasa majeno mengi makubwa ya wagiriki



hutumia alama ya ngao ya kichwa cha medusa kama kinga ya mambo mabaya

Uzuri Umemponza medusa mpaka aonekane chukizo na hatarii kwa viumbe wengine,

lakini pamoja na kuwa hatari kwa watu na kwenda kujificha kusikojulikana ,bado kuna watu pia walimfata kuuhitaji pia

ule ubaya wake,kujilinda kwake kwa maadui ndo kama kujiwekea stori mbaya kwa watu.

na hvyo ndivyo dunia ilivyo.vyovyote utavyokuwa au chochote utakachokuwa nacho,kiwe kibaya au kizuri lazima kuwe

na watu wakukupenda au wakukuchukia, lazima kuwe na watu wa kukudhuru au wakukusaidia.

Asante kwa kuwa pamoja