Wednesday, February 17, 2021

ZIJUE FAIDA ZA LIMAO

 HILO NDO LIMAO

Muhimu ni kuliandaa vizuri na kufata maelekezo

Leo ningependa kuwapa kitu tofauti kidogo
Kila mtu analijua limao na faida zake zipo nyingi  tu, ikiwemo kutumika kutengenezea dawa za tiba mbalimbali
mfano tiba ya ngozi,tiba ya kifua na nyingine nying nyingnezo.lakini leo nakuonesha  faida 
tatu tu kutoka kwenye limao
Lakufahamu kwanza limao ni tunda lenye umaji maji wa acid, yaani ni tunda lenye citric acid
na uwingi wa vitamin c

Kukata harufu ya kikwapa
Huu ni mbadara mkubwa wa matumizi ya deodorant ambazo ni chemical na pia
hufubaza nguo katika maeneo ya kwapa kwa kiwango kikubwa
unachotakiwa kufanya ni kukata kipande kidogo tu cha limao na kupaka kwapani
subiria bila kusafisha kwa dakika tano mpaka kumi kisha nawa au nenda kaoge
hutokaa na kusikia haruf ya kikwapa zaidi ya siku tano. ,unaweza paka tena baada hata ya siku tatu
usitumie njia hii baada ya kushave

Unaweza fanya hivyo hvyo katika maeneo mengine ya mwili ambayo unaona 
yanatoa harufu mbaya,unaweza fanya hayo bila shida yoyote na ikakupa matokeo
 mazuri tu.
Kusafishia aina zote za chuma
Kusafisha vitu vya chuma ambavyo uchafu umegandiaa, mfano ule uchafu wa jikoni
uchafu unaonata ,uliochanganyika na mafuta mfano mafuta mafuta ya samaki

Katika hili kuna cha ziada inabd uwe nacho ,baking powder

Andaa baking powder hiz za kawaida za Simba, andaa na limao lako.
Sambaza unga wa baking powder katika eneo unalotaka kusafishaa,kamua limao 
katika chombo kisha umiminie,au kamulia limao moja kwa moja katika sehem uliyosambaza
unga wa baking powder  ,subiria kwa dakika tano,kisha anza kusafisha kwa brush tu la kawaida la vyombo

ukimaliza hapo unaweza ukafuta tuu na kitambaa safi na sabuni

Kulainishiaa maeneo ya mwili
Tatu ni katika kulainisha maeneo katika mwili ambayo kidoogo yamekakamaa
mfano kama  nyayo za miguu yako zimekakamaaa ,unaweza kutumia limao kufanya unyayo ukawa
soft/laini  tena
unachotakiwa kufanya ni rahisi tu chagua siku au muda ambao hauna shughuli ya kufanya
angalau kwa sekunde 30,kata vipande vipande vidogo dogo  vya malimao na maganda yake
kisha weka chini ya unyayo  valia na soksii tulia kwa dakika 30 ,unaweza tumia muda huo kuangalia movie 
ama maigizo mbali mbali  baada ya hapo toa kanawe miguu yako ,utanishukuru baadaae 

Kama vitamin C katika kupambana na kinga ya mwili
Limao lina kiwango kikubwa cha vitamin C inayoweza kusaidiia kuinua kinga ya mwili na kupambana na maradhi aina nying 
yanayosababishwa na upungufu wa vitamin C ikiwemo mafua

0 comments:

Post a Comment