Tuesday, September 19, 2017

IJUE SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI

Unapozungumzia Binaadam na viumbe wengine ambao huanza maisha kwa kuzaliwa bila shaka kabisa mwanamke ndio kiungo muhimu katika kufanikisha Jambo zima,Kutokana na hilo wanawake ni moja ya makundi muhimu katika jamii yetu. Mwanamke ni mama, na ndiye kiumbe pekee ambaye hufanya kazi ya kuleta uhai duniani.



Lakini mwanamke huyu hivi sasa yu mashakani, kwani ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi umeshika kasi nchini, hivyo hutesa na hatimaye kuua maelfu ya wanawake.Saratani ni mfumo au tabia ya chembe hai nyeupe kukua katika sehemu ya mwili wa binadamu katika mfumo usio wa kawaida.

Hivyo basi, chembe hizo zikikua katika shingo ya kizazi cha mwanamke, kinyume cha taratibu, hiyo huitwa saratani ya shingo ya kizazi.

Dk Henry Mwakyoma, Daktari Bingwa wa Kitengo cha Patholojia katika hospitali ya Muhimbili, amefanya utafiti kati ya Februari 2001 na Februari 2002. Lengo la utafiti huo lilikuwa ni kuangalia ukubwa wa tatizo la saratani ya shingo ya kizazi kwa hapa nchini.

Aliwapima wanawake 224 kutoka mikoa mbalimbali nchini waliopewa rufaa ya kufika Muhimbili. Katika wagonjwa hao, 193, sawa na asilimia 86.2 waligundulika kuwa na saratani ya shingo ya kizazi na 31 sawa na asilimia 13.8 walikuwa hawana saratani.

Dk Mwakyoma anasema, miongoni mwa waliokutwa na saratani hiyo, walikuwa na umri wa kuanzia miaka 24 hadi 82.

"Katika hao walioathirika zaidi walikuwa ni wenye umri wa miaka 40 hadi 49 na wengine walikuwa na umri wa chini ya miaka 40," anasema Mwakyoma.
Daktari bingwa huyu alifanya utafiti mwingine kuhusu saratani ya aina hii kati ya mwaka 1980 hadi 1984 katika nchi za Tanzania na Uswisi. Lengo lilikuwa kuangalia ukubwa wa tatizo hili katika nchi zinazoendelea na zilizoendelea.

Utafiti ulifanyika katika hospitali kuu za rufaa Tanzania, ambazo ni Bugando, KCMC, hospitali ya rufaa ya Mbeya na Muhimbili.

"Niliamua kufanya utafiti huo katika hospitali za rufaa nchini ili kupata namba ya wagonjwa katika mikoa mikubwa," anasema Dk Mwakyoma.

Matokeo ya utafiti huo yalionyesha kuwa, katika hospitali ya KCMC asilimia 13.9 ya wanawake waliopimwa waligundulika na saratani ya shingo ya kizazi. Bugando, asilimia 20, Mbeya asilimia 24.3, na Muhimbili walikuwa ni asilimia 18.4 ya wanawake.
"Katika aina kumi za saratani duniani, basi saratani ya shingo ya kizazi ndiyo inayoongoza kwa kuwaathiri wanawake hapa nchini," anasema Dk Mwakyoma.

Chanzo cha saratani hii
Dk Mwakyoma anabainisha kuwa, sababu kubwa ambayo hupelekea wanawake wengi kupata saratani ya shingo ya kizazi ni matokeo ya ufanyaji wa ngono.

"Kufanya ngono ninaweza kusema ni sababu kubwa na sababu nyinginezo huambatana na hizo lakini kichocheo kikubwa ni ngono," anasema.

Anasema, sababu nyingine zinazosababisha mwanamke kupata saratani hii ni kufanya mapenzi katika umri mdogo. Wanawake wengi wanaofanya mapenzi chini ya miaka 16, wapo katika hatari kubwa.
"Katika wanawake waliogundulika na saratani, asilimia 14.95 kwa wastani walikuwa wameanza kufanya mapenzi wakiwa na umri wa miaka 14 hadi 25," anafafanua Dk Mwakyoma.

Asilimia 17.8 ya wanawake hao, walikuwa wameolewa wakiwa na umri wa kuanzia miaka 11 hadi 35.
Hali kadhalika kati ya wanawake 161, 71 (44%) ya waliopimwa na kugundulika na saratani ya shingo ya kizazi, waliolewa wakiwa chini ya umri wa miaka 18.

Sababu nyingine inayosababisha saratani ya shingo ya kizazi ni mimba na kuzaa. Dk Mwakyoma anasema, idadi ya ujauzito kwa wanawake husababisha saratani ya shingo ya kizazi.

Kwa mfano, mtu ambaye amebeba ujauzito zaidi ya mara sita (kwa hapa nchini) yupo katika hatari ya kupata saratani ya aina hii.

"Katika wanawake 193 niliowapima, 136 waliwahi kupata mimba zaidi ya mara nne, nasisitiza si kuzaa, yaani wastani wa mimba ulikuwa ni saba," anasema.Katika kiwango cha kimataifa, wastani wa kubeba mimba usio katika hatari ya kusababisha saratani ya shingo ya kizazi ni mara nne.

"Sababu nyingine ni kiwango cha kuzaa, wanawake wanaozaa sana huwa katika hatari, kwa mfano katika wanawake 193 niliowafanyia utafiti, 107 walikuwa na watoto zaidi ya wanne," anasema.

Anasema, idadi ya wapenzi ni sababu nyingine. Mwanamke mwenye wapenzi wengi, bila shaka atakuwa anafanya mapenzi kwa kiwango kikubwa, hivyo basi kupata magonjwa ya zinaa yanayosababisha saratani hii ni rahisi.
Vilevile wanawake walioolewa mara nyingi nao wamekuwa wakigundulika na saratani ya shingo ya kizazi. Kwa mfano, wenye historia ya kupewa talaka kisha kuolewa tena, au wajane wanaoolewa kwa mara nyingine na wanaotengana na wapenzi katika vipindi tofauti tofauti.

"Wapo wanaume hatari ambao nao huchangia wanawake kupata saratani ya shingo ya kizazi, hawa kitaalamu tunawaita High Risk Male Sexual Partner' hawa wanapokuwa na wapenzi wengi hutokea wakawaambukiza wanawake magonjwa ya zinaa."

Dk Mwakyoma anaongeza kuwa, ugonjwa wa zinaa ambao ndicho kichocheo kikuu cha saratani ya shingo ya kizazi ni Human Papiloma Virus 16 na 18 (HPV).Ugonjwa huu unapokomaa huzalisha seli ambazo hukua kinyume na utaratibu na kuanza kushambulia sehemu ya shingo ya kizazi.

Jambo lingine linalosababisha saratani ya shingo ya uzazi ni usafi katika sehemu za siri za mwanamke. Wanawake wanaofanya usafi sehemu zao za siri kwa kutumia bidhaa au baadhi ya vifaa visivyofaa kutumiwa ukeni huweza kupata saratani hii. Kwa mfano, bidhaa zenye kemikali ya coal tar,' ambayo mara nyingine huwekwa kwenye sabuni ama manukato.

Dalili
Dk Mwakyoma anasema, ni vyema na muhimu mno kwa wanawake kupima afya zao za uzazi kabla ya kuona dalili.


Mwanamke anapoona dalili basi saratani huwa imefikia hatua mbaya ya kifo. Anasema hatua hizi zipo katika makundi ambayo yamegawanyika.
"Ipo hatua ya mwanzo (pre-invasive) ambapo saratani bado haijafanya mashambulizi katika mwili kwa asilimia kubwa na hatua ya pili (invasive) ambayo imegawanyika katika hatua nne na hatua hii saratani huwa imeshasambaa katika sehemu nyingine za mwili," anasema.

Anazitaja dalili kuu za ugonjwa huu kuwa ni kutokwa na damu kwa wingi hasa wakati wa hedhi. Nyingine ni kutoa maji maji yenye harufu mbaya ukeni, na kupata maumivu sambamba na kutoka damu baada ya kufanya tendo la ndoa.
Dk Mwakyoma anatoa ushauri kwa serikali kuwa, itungwe sera ambapo ni lazima kila mwanamke aliye katika umri wa kufanya mapenzi akapimwe saratani ya shingo ya kizazi.

"Ili kupunguza tatizo ni bora kuwapima, tunatumia kipimo cha pap-smear' ambacho hata Uswisi hutumia kuwapima wanawake," anasisitiza

Naye Dk Innocent Mosha, wa kitengo cha patholojia Muhimbili anasema, ni vyema wasichana wadogo wafuate maadili na wajiepushe na vitendo vya ngono katika umri mdogo ili kujiepusha na maradhi haya.

Takwimu za mwaka 2010 kutoka Shirika la Afya Duniani, (WHO) zinasema, kwa Tanzania wastani wa wanawake 6,241 huugua saratani ya shingo ya kizazi kila mwaka na 4355 kati yao hupoteza maisha.

Sunday, September 17, 2017

MAKONDA ATANGAZA NEEMA YA VIWANJA/HOTUBA

RC MAKONDA ASHUSHA NEEMA KWA WATUMISHI WA UMMA DAR ES SALAAM HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM KWA WATUMISHI WAKE NA WANANCHI WA MKOA WA DAR ES SALAAM.

Watumishi wa Manispaa zote, idara za AFYA (wauguzi, madaktari, maafisa afya), ELIMU  (walimu Shule za Msingi, na sekondari, waratibu wa elimu kuanzia kata, wilaya na Mkoa,  Askari wa Vikosi vyote Jeshi la Polisi(kanda maalum, mikoa ya Kipolisi temeke, kinondoni, ilala, Ubungo, kigamboni, na wilaya zake), Magereza, na uhamiaji, Jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ na kikosi cha Zima moto
DONDOO MUHIMU ZA HOTUBA
Kila MTUMISHI anaefanyakazi kazi Chini ya Serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam  KUPEWA  kiwanja cha  UJENZI WA MAKAZI YA KUDUMU.kwa Gharama ya Square Mita moja kwa shilingi elfu nne (4,000 Tsh) badala ya square Mita moja kwa Shilingi elfu kumi na Tano (15,000 Tsh).Malipo Ndani ya Miaka Mitano (5) Mtumishi Ruksa Kujenga na Kulipa taratibu Ndani ya Miaka mitano.Vibali vya Ujenzi BURE uku Mkipewa KIPAUMBELE.Ndugu zangu WATUMISHI, nikiwa Msaidizi wa Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, dkt. John Magufuli* amenipa Dhamana ya Kuongoza Mkoa wa Dar es Salaam, mimi na timu yangu tutaendelea kushughulika na kutatua changamoto mbalimbali ambapo natambua ziko changamoto za Kimazingira zinazowagusa wafanyakazi mfano Sekta ya afya kutokuwa na wodi za kulaza Wagonjwa, upande wa Polisi kutokuwa na vitendea kazi mfano magari ya kutosha, upande wa Walimu kutokuwa na ofisi, upande wa michezo kutokuwa na viwanja vya michezo. Kwa upande wa wananchi tumeona masuala ya migogoro ya Ardhi, haya yote ni Majukumu yetu sisi kama viongozi na wawakilishi wa Rais ambae alitoa ahadi wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 ambapo wananchi walimpa ridhaa ya kuliongoza taifa hili kama Rais wao na amiri Jeshi mkuu. Ndugu zangu WATUMISHI,natambua ziko changamoto zinazowahusu watendaji wetu, ni kweli tutajenga *WODI*, tutajenga OFISI, ni kweli tutaleta magari ya polisi lakini swali bado litabaki mtumishi huyu wa kawaida alieko kwenye sekta ya afya ambae hana muda wa kufanya kasi zingine za kujiongezea kipato kutokana na kutokuwa na Muda, je maisha yake na kipato chase yanampa matumaini na MORARI ya kufanya kazi kwa ufanisi? mwalimu ambae anaangaika na watoto wetu ili wafaulu vizuri kuanzia asubuhi mpaka jioni na kusahihisha madaftari yao na hapo hapo anatakiwa kuandaa somo la kesho, hivi atapata atapata muda wa kufanya Biashara ya KARANGA na kupata faida? Hebu tafakari Askari polisi wetu polisi wa nafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha usalama utakuwepo katika mkoa, Hebu tafakari Muuguzi ambae ni MKUNGA analazimika kukesha KUZALISHA wake zetu na kutunza vichanga vyetu hivi huyu anapata Muda Gani wa kufanya biashara? Hata kama wakichukua MIKOPO katika taasisi mbalimbali wanajikuta wanashindwa Kurejesha kwa sababu biashara zao zinasimamiwa na Ndugu ambao hawana UZOEFU wanajikuta biashara zinakufa na wanapata mzigo mkubwa wa KULIPA MADENI kwa riba kubwa sana na kujikuta MITAJI imekata haya ni maswali magumu kwangu kuyajibu, kwani hata akitoka nje kwenda kuuziwa bidhaa atanunua kwa bei ya soko Hatauzwi kwa bei ya chini kwa kuwa yeye ni mwalimu, au polisi au muuguzi, atauziwa sawa na mfano wa mfanyabiashara Biashara, mwanasiasa atauziwa bei moja tu licha ya kuwa hawa watu wawili wanatofautiana kipato na aina ya kazi ila wanauziwa bei sawa hii sio sawa kwa Watumishi wangu. Ndugu zangu *WATUMISHI*, kutokana na sababu hizo na nyingine nyingi, nimeona mimi kama msaidizi wa *Mhe, Rais, dkt. John Magufuli* iko *HAJA na TIJA* kuanza sasa na *KUGUSA* na maisha ya watendaji Mmoja mmoja na kumpa *FAHARI* ya yeye kama Mwalimu, muuguzi au polisi ili anaporejea nyumbani mtoto wake nae atamani kuwa Mwalimu au Muuguzi, au Daktari kwa sababu anaona *FAHARI* mzazi wake anayopewa katika utumishi wake kwa wananchi. Ndugu zangu *WATUMISHI,* nimetafakari na kufikiria sana katika njia sahihi ya *KUWAKOMBOA* Watumishi hawa na kwa kuanzia na kuwapatia *VIWANJA VYA KUJENGA NYUMBA ZA KUISHI* (makazi), katika utekelezaji wa jambo hili Nimefanya mazungumzo na WADAU mbalimbali pamoja na WAPIMAJI wakubwa wa viwanja, kuangalia Bei ya SOKO ambayo inatofautina, mana natambua yako maeneo yanauzwa viwanja vilivyopimwa kwa Gharama ya Elfu ishirini na tano (25,000) kwa Square Mita moja na bei ya soko inakwenda mpaka shilingi elfu kumi na mbili (12,000) kwa square Mita moja. Hatua hii imesababisha Watumishi wengi kushindwa kumudu kununua Viwanja katika maeneo mazuri yaliyopimwa Hatua ambayo imesababisha baadhi yao kujenga nyumba katika maeneo yasiyostahili na kujikuta  WANABOMOLEWA.Ndugu zangu *WATUMISHI, NAOMBA NITANGAZE RASMI KWA WATUMISHI WANGU KUWA NIMEFANIKIWA KUWASHAWISHI WATU WENYE MAENEO MAKUBWA NA WAPIMAJI WAKUBWA WA VIWANJA NA KUFANIKIWA KUFANYA MAJADILIANO NAO KWA KINA NA KUPATA VIWANJA KATIKA MAENEO MBALIMBALI YALIVYOPIMWA AMBAVYO VITAUZWA KWA SQUARE MITA MOJA SHILINGI ELFU NNE TU (4,000 Tsh) badala ya shilingi elfu kumi na tano (15,000 Tsh) kwa Square Mita.Ndugu zangu WATUMISHI, viwanja hivi *VIPO TAYARI KWA AJILI YENU* na tayari nimeshaelekeza Viongozi wenu Kamanda wa Kanda maalum ya Dar es salama, Afisa Uhamiaji wa Mkoa,Afisa Magereza wa Mkoa, Mganga Mkuu wa Mkoa, Afisa *ELIMU* mkuu wa mkoa, Wakurugenzi wote wa Manispaa, wakuu wa wilaya *KUWAELEZA* Watumishi wao na kuwakutanisha Watumishi wao na WAHUSIKA WA viwanja hivyo kwa ajili ya kuanza UTEKELEZAJI.Ndugu zangu *WATUMISHI*, pamoja na kuuziwa viwanjwa hivyo kwa Square Mita moja kwa shilingi elfu nne, _Mhe Makonda_ pia *AMEAGIZA* kama Mtumishi Hana Fedha za Kulipa kwa wakati mmoja *APEWE* muda wa Kulipa ndani ya *miaka mitano (5),* ambapo amesema endapo Mtumishi atahitaji kuanza ujenzi kabla ya kukamilisha MALIPO _Mhe Makonda_ *AMEELEKEZA* mtumishi huyo *ARUHUSIWE* kuendelea na Ujenzi na Atalipa taratibu taratibu uku akiendelea na Ujenzi. Mwisho _Mhe Makonda_ *AMEWAELEKEZA* Wakurugenzi wa Manispaa *ZOTE* katika Mkoa wa Dar es Salaam kuwapa *KIPAUMBELE* katika utoaji wa *VIBALI* (bure) vya Ujenzi wa Makazi ya Kudumu pasipo kutoa *FEDHA* yoyote. Mhe Makonda_ amesema *LENGO* na *NIA* ya serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam ni kuleta *HESHIMA* na kutoa *UTUMISHI* iliotukuka kwa Watumishi wote wa Mkoa wa Dar es Salaam Chini ya Uongozi wa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa *Mhe, dkt. John Magufuli.Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Dar es Salaam, Mungu Mbariki na Kumlinda Rais, Dkt. John Pombe Magufuli.
ASANTENI KWA KUNISIKILIZA.*

CHANZO CHA MOTO NYUMBA YA ZITO KABWE



Siku moja baada ya tukio la kuungua kwa nyumba ya mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe iliyopo katika eneo la Kibingo kata ya Mwandiga mkoani humo, Jeshi la Polisi limetoa ufafanuzi kuhusiana na chanzo cha moto huo pamoja na mali zilizoteketea. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha moto huo ni betri za umeme wa jua zilizokuwa ndani kuzidiwa nguvu na kisha kulipuka. Aidha, Kamanda Mtui amesema bado jeshi hilo linaendelea na uchunguzi wa kina na kutoa wito kwa wananchi kuwa na utamaduni wa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye mifumo yao ya umeme ili kutoa taarifa mapema kwenye mamlaka husika pindi wanapohisi uwepo wa hitilafu yeyote
TBC habari